KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 29, 2012

Yanga kukata utepe na Atletico Kombe la Kagame

KATIBU Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye.



MABINGWA watetezi Yanga watafungua dimba la mechi za michuano ya soka ya Kombe la Kagame kwa kumenyana na Atletico ya Burundi.
Ratiba ya michuano hiyo iliyotangazwa jana na Katibu Mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Nicholas Musonye inaonyesha kuwa, mechi hiyo itapigwa Julai 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ratiba, pambano hilo litakaloanza saa 10 jioni, litatanguliwa na pambano lingine kati ya APR ya Rwanda na Wau Salaam ya Sudan Kusini.
Yanga imepangwa kundi C pamoja na timu za APR, Wau Salaam na Atletico.
Kundi A linaundwa na timu za Simba ya Tanzania Bara, URA ya Uganda, Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Ports ya Djibouti.
Azam imepangwa kundi B pamoja na timu za Mafunzo ya Zanzibar na Tusker ya Kenya. Timu 11 zinatarajiwa kushiriki kwenye michuano hiyo.
Ratiba inaonyesha kuwa, timu tatu za kwanza kutoka kundi A na C na timu mbili kutoka kundi B zitafuzu kucheza hatua ya robo fainali. Mechi za hatua hiyo zitachezwa Julai 23 na 24, mechi za nusu fainali Julai 26 wakati fainali na mechi ya kutafuta mshindi wa tatu itapigwa Julai 28.
Ratiba kamili ni kama ifuatavyo:

Julai 14, 2012- APR vs Wau Salaam Taifa C Saa 8

Yanga vs Atletico Taifa C Saa 10

Julai 15, 2012 Azam vs Mafunzo Chamazi B Saa 10

Julai 16, 2012 Vita Club vs Ports Taifa A Saa 8

Simba vs URA Taifa A Saa 10

Julai 17,2012 Atletico vs APR Taifa C Saa 8

Walau Salaam vs Yanga Taifa C Saa 10

Julai 18,2012 Vita Club vs URA Taifa A Saa 8

Ports vs Simba Taifa A Saa 10

Julai 19,2012 Atletico vs Walau Salaam Taifa C Saa 8

Mafunzo vs Tusker Taifa B Saa 10

Julai 20, 2012 Ports vs URA Taifa A Saa 8

Yanga vs APR Taifa C Saa 10

Julai 21, 2012 Azam vs Tusker Taifa B Saa 8

Simba vs Vita Club Taifa A Saa 10

No comments:

Post a Comment