KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, June 30, 2012

Yanga mpya yaanza kuonyesha cheche

Timu ya soka ya Yanga jana iliichapa Express mabao 2-1 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Yanga tangu ilipokamilisha usajili wa msimu wa 2012/2013 na iliwachezesha wachezaji wake kadhaa wapya wakiwemo kipa Ally Mustafa, beki Kevin Yondani na kiungo Frank Domayo.

Mshambuliaji Jerry Tegete ndiye aliyewajaza furaha mamia ya mashabiki wa Yanga waliofurika kwenye uwanja huo, ambao walikuwa na hamu kubwa ya kuiona timu yao mpya, ambayo ilikuwa chini ya Kocha Fred Felix Minziro.

Jerry aliifungia Yanga mabao hayo mawili baada ya kucheza kwa uelewano mkubwa na Saidi Bahanuzi, Nizar Khalfan na Simon Msuva, ambaye alikuwa nyota ya mchezo.

Express ilizinduka katika kipindi cha pili baada ya kufanya mabadiliko kadhaa ya wachezaji na kufanikiwa kupata bao la kujifariji baada ya beki mmoja wa Yanga kujifunga alipokuwa katika harakati za kuokoa mpira wa kona.

Katika mechi hiyo, Yanga ilionyesha uhai kwenye safu yake ya ulinzi iliyokuwa chini ya Yondani, Nadir Haroub, Juma Abdul na Oscar Joshua huku kiungo mkongwe, Athumani Iddi na chipukizi Domayo wakicheza vizuri kwenye safu hiyo.

No comments:

Post a Comment