KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 27, 2012

Dodoma yaitambia Mbeya Copa Coca Cola

TIMU ya soka ya Dodoma ya vijana wa chini ya miaka 17 imeendeleza wimbi la ushindi kwenye michuano ya Copa Coca-Cola baada ya kuifunga Mbeya mabao 2-0.
Mechi hiyo ya kundi C iliyokuwa ya kusisimua na yenye ushindani mkali, ilichezwa jana asubuhi katika uwanja wa Tamco uliopo Kibaha mkoani Pwani.
Katika mechi hiyo, mabao ya Dodoma yalifungwa na Japhet Lunyungu dakika ya 59 na Frank Kaji dakika saba kabla ya mchezo kumalizika.
Nayo Mjini Magharibi ilitoka uwanjani kifua mbele baada ya kuifunga Iringa mabao 3-0 katika mechi ya kundi B iliyochezwa kwenye uwanja wa Nyumbu mkoani Pwani.
Mechi za asubuhi zilizokuwa zichezwe leo kati ya Arusha na Kusini Pemba kwenye uwanja wa Tanganyika Packers na Pwani na Tabora kwenye uwanja wa Karume, zilitarajiwa kuchezwa mchana kutokana na kutokuwepo kwa mawasiliano ya barabara kutoka Pwani kuingia Dar es Salaam.
Leo jioni kutakuwa na mechi kati ya Rukwa na Ruvuma (Tanganyika Packers), Mwanza na Tanga (Nyumbu), Kaskazini Unguja na Mara (Tamco) na Singida na Kagera (Karume).

No comments:

Post a Comment