KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, June 27, 2012

Simba yamtema Jabu, yamtoa mkopo Haruna

KLABU ya Simba imetangaza rasmi kuwaacha wachezaji wake wanne katika msimu ujao wa ligi na kuwatoa kwa mkopo wengine wanne kwa klabu zingine.
Simba imewasilisha majina hayo juzi kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ikiwa ni utekelezaji wa kanuni za shirikisho hilo zinazotaka kila klabu itangaze mapema majina ya wachezaji inaowaacha.
Mabingwa hao wa Tanzania Bara ni miongoni mwa klabu tano za ligi hiyo zilizowasilisha majina hayo TFF juzi.
Wachezaji, ambao Simba imetangaza kuwaacha katika usajili wa msimu ujao ni Ally Mustafa, Derick Walulya, Gervas Kago na Juma Jabu wakati mkataba wa Salum Kanoni unatarajiwa kumalizika Juni 30 mwaka huu.
Kwa mujibu wa orodha hiyo, Simba imewatoa kwa mkopo Rajabu Isihaka, Salum Machaku, Haruna Shamte na Shija Mkina.
Polisi Morogoro, iliyopanda daraja msimu huu, imewaacha wachezaji 17 wakati Tanzania Prisons ambayo pia imepata hadhi ya ligi kuu msimu huu, imewaacha wachezaji 11.
Habari zaidi kutoka ndani ya TFF zimeeleza kuwa, Azam imekatisha mikataba ya wachezaji watatu wakati wachezaji 12 wamemaliza mikataba yao katika klabu ya Kagera Sugar.
Uhamisho wa wachezaji kwa msimu huu ulianza Juni 15 mwaka huu na utamalizika Julai 30 mwaka huu wakati kipindi cha kuanza kwa usajili kwa wachezaji wasio wa ligi kuu ni kati ya Juni 15 na 30 mwaka huu.
Wachezaji walioachwa na Polisi Morogoro ni Abdul Ibadi, Ally Moshi, Benedict Kitangita, Hassan Kodo, Hussein Lutaweangu, Hussein Sheikh, Juma Maboga, Mafwimbo Lutty, Makungu Slim na Mbaraka Masenga.
Wengine ni Method Andrew, Moses Mtitu, Ramadhan Kilumbanga, Ramadhan Toyoyo, Said Kawambwa, Salum Juma na Thobias John.
Tanzania Prisons imewaacha Adam Mtumwa, Dickson Oswald, Exavery Mapunda, Ismail Selemani, Lwitiko Joseph, Mbega Daffa, Mwamba Mkumbwa, Musa Kidodo, Rajab Ally, Richard Mwakalinga na Sweetbert Ajiro.
Wachezaji waliomaliza mikataba yao kwa mujibu wa Kagera Sugar ni Cassian Ponera, Hamis Msafiri, Hussein Swedi, Ibrahim Mamba, Martin Muganyizi, Mike Katende, Moses Musome, Msafiri Davo, Said Ahmed, Said Dilunga, Steven Mazanda na Yona Ndabila.
Azam imewasitishia mikataba wachezaji Tumba Swedi, Mau Bofu na Sino Augustino.

No comments:

Post a Comment