KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, June 11, 2012

30 waingia kozi ya kujenga afya ya FIFA

Walimu 18 wa shule za msingi na makocha 12 wa mpira wa miguu
wanashiriki kozi ya mpango maalumu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa
Miguu (FIFA) kwa ajili ya kujenga afya kupitia mpira wa miguu.
Kozi hiyo ya siku tano inayoitwa FIFA 11 for Health imeanza leo (Juni 11
mwaka huu) kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na
itamalizika Juni 15 mwaka huu.
Mafunzo hayo yanaendeshwa na wakufunzi kutoka FIFA ambapo ujumbe katika 11 for Health ni 1. Cheza mpira, 2. heshimu wasichana na wanawake, 3. jikinge na virusi vya Ukimwi (HIV), 4. epuka dawa za kulevya, pombe na sigara, 5. tumia neti zenye viuatilifu, 6. nawa mikono yako, 7. kunywa maji salama, 8. kula chakula chenye mpangilio, 9. pata chanjo, 10. tumia dawa
sahihi na 11. cheza mchezo mzuri.
Walimu hao kutoka shule za Mkoa wa Dar es Salaam ni Aloyce Rutta
(Montfort, Temeke), David Kazinge (Temeke, Temeke), Rajabu Ased (Mtoni
Kijichi, Temeke), Mathew Kambona (Mji Mwema, Temeke), Ruth Mahenge
(Chang’ombe, Temeke), Abdul Mikoroti (Nzasa, Temeke), Exuperus Kisaka
(Mavurunza, Ilala), Khadija Kambi (Karume, Ilala) na Hamisi Ibrahim
(Tusiime, Ilala).
Wengine ni Baltazar Kagimbo (Tabata Jica, Ilala), Isaac Mhanza (Airwing,
Ilala), Baraka Baltazar (Muhimbili, Ilala), Job Ndugusa (Upanga, Ilala),
Tumaini Hiluka (Buguruni, Ilala), Maua Rashid (Uhuru Wasichana, Ilala),
Mussa Kapama (Bunju A, Kinondoni), Raymond Rupia (St. Anne Maria,
Kinondoni) na Priscus Shilayo (JK Nyerere, Kinondoni).
Kwa upande wa makocha ni Dismas Haonga, Frank Mwakang’ata, John
Sebabili, Michael Bundala, Peter Manyika, Raphael Matola, Renatus Magolanga,
Robert Mayunga, Said Pambaleo, Seba Nkoma Titus Michael na Wilfred Kidao. Programu hiyo inalenga watoto ambapo washiriki watakaofaulu katika kozi hiyo ndiyo baadaye watakuwa wakufunzi kwa ajili ya kuifanya katika maeneo mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment