KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

SIMBA YATANGAZA NYOTA 18 WANAOKWENDA ANGOLA KESHO




WAWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya soka ya klabu bingwa Afrika, Simba wanaondoka nchini leo kwenda Angola kwa ajili ya mechi yao ya marudiano ya raundi ya kwanza dhidi ya Recreativo Libolo.

Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, timu hiyo itakwenda Angola ikiwa na msafara wa wachezaji 18 na viongozi saba.

Kamwaga alisema Simba inatarajiwa kuondoka saa 11.10 alfajiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways) na inatarajiwa kuwasili Luanda saa nne asubuhi.

Aliwataja wachezaji watakaokuwemo kwenye msafara wa timu hiyo kuwa ni Juma Kaseja, Abel Dhaira, Nassor Masoud, Amir Maftah, Koman Bili Keita, Juma Nyoso, Shomari Kapombe, Salim Kinje, Ramadhani Chomboh, Amri Kiemba, Haruna Moshi, Kiggi Makasi, Abdallah Seseme, Amri Kiemba, Haruna Chanongo, Mrisho Ngassa, Felix Sunzu na Abdallah Juma. Viongozi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia

Hanspope, mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Muhsin Balhabou, Kocha Mkuu, Patrick Liewig, msaidizi wake, Jamhuri Kihwelo, Daktari wa timu, Cosmas Kapinga, kocha wa makipa, James Kisaka na mtunza vifaa Kessy Rajab.

Kwa mujibu wa Kamwaga, timu hiyo ilitarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho jana jioni kabla ya kwenda kambini, ambako watapumzika kwa muda kwa ajili ya kusubiri muda wa safari.

Pambano kati ya Simba na Libolo limepangwa kufanyika keshokutwa katika uwanja wa Calulo uliopo katika mji mdogo wa Calulo kwenye Jimbo la Kwanza Kusini.

Katika mechi ya awali iliyochezwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Libolo iliichapa Simba bao 1-0. Ili isonge mbele katika michuano hiyo, Simba italazimika kuishinda Libolo mabao 2-0.

Kamwaga alisema licha ya kufungwa katika mechi ya awali, matumaini ya Simba kusonga mbele ni makubwa kutokana na maandalizi waliyoyafanya.

No comments:

Post a Comment