KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 24, 2013

SIMBA YAANGUKIA PUA KWA MTIBWA


MATUMAINI ya Simba kutetea ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara leo yameendelea kuyeyuka baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mtibwa Sugar.


Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wachezaji wa Simba tangu mwanzo hawakuonekana kucheza kwa kujituma na hivyo kutoa mwanya kwa Mtibwa kutawala.

Bao pekee na la ushindi la Simba lilipachikwa wavuni na beki Salvatory Ntebe, aliyepanda mbele kusaidia mashambulizi. Alifunga bao hilo baada ya kuunganisha wavuni krosi kutoka kwa Vicent Barnabas.

No comments:

Post a Comment