KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

GIGGS AWEKA REKODI YA KUCHEZA MECHI 999



LONDON, England
WAKATI Ryan Giggs alipoifungia Manchester United bao la ushindi katika mechi ya ligi kuu ya England dhidi ya QPR na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, alikuwa ameweka rekodi ya kucheza mechi 999.

Mwanasoka huyo mkongwe anaweza kuweka rekodi ya kucheza mechi 1,000 keshokutwa wakati Manchester United itakapomenyana na Norwich City katika mechi ya ligi hiyo.

Giggs ni jina kubwa katika kikosi cha sasa cha Manchester United. Ni mchezaji aliyeanza kuichezea klabu hiyo tangu Machi 2, 1991, wakati ambao baadhi ya wachezaji alionao sasa aidha walikuwa na umri mdogo au hawajazaliwa.

Mbali na rekodi hiyo, wiki chache zijazo, Giggs anaweza kuongeza mataji na medali akiwa na kikosi cha Manchester United, ambacho kinapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England msimu huu.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Wales aliichezea Manchester United kwa mara ya kwanza katika mechi ya ligi dhidi ya Everton. Mechi hiyo ilipigwa Machi 2, 1999.

Wakati Giggs akiteremka dimbani kucheza mechi hiyo, mkongwe mwenzake, Paul Scholes alikuwa na umri wa miaka 16 na miezi minne wakati Rio Ferdinand alikuwa na umri wa miaka 12 na miezi minne na huenda walikuwa sekondari.

Katika kipindi hicho, wachezaji kama David de Gea na Danny Welbeck walikuwa bado hawajaanza hata kutembea wakati Phil Jones na Nick Powell walikuwa hawajazaliwa.

Nahodha wa zamani wa Manchester United, Roy Keane, David Beckham na Gary Neville walicheza pamoja na Giggs kwenye kikosi cha timu hiyo na kuondoka wakimwacha bado tegemeo kubwa.

Manchester United ilitumia pauni milioni 50 msimu huu kuwasajili Ashley Young, Nani na Shinji Kagawa, ambao wanacheza nafasi moja na Giggs wakati Tom Cleverley na Anderson pia wanapigania namba kwenye nafasi hiyo na nahodha huyo wa zamani wa Wales.

Kocha Mkuu wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amekuwa na utamaduni wa kuwaamini wachezaji wake wakongwe na hivyo ndivyo anavyofanya kwa Giggs.

Iwapo Giggs atafanikiwa kuweka rekodi ya kucheza mechi 1,000 msimu huu, atakuwa mchezaji wa saba nchini England kufanya hivyo. Wachezaji waliowahi kuweka rekodi hiyo ni Peter Shilton, Ray Clemence, Pat Jennings, David Seaman, Tony Ford na Graham Alexander.

Wachezaji wengine walioweka rekodi ya kucheza mechi nyingi katika ligi kuu ya England ni Alan Shearer (797) na Eric Cantona (453).

UMRI WA WACHEZAJI WA MAN UTD ULIVYOKUWA WAKATI
GIGGS ALIPOANZA KUICHEZEA TIMU HIYO MACHI 2, 1999

Paul Scholes, miaka 16 na miezi minne
Anderson, miaka miwili na miezi 11
Rio Ferdinand, miaka 12 na miezi minne
Javier Hernandez, miaka miwili na miezi minane
Michael Carrick, miaka tisa na miezi minane
Alexander Buttner, miaka miwili na mwezi mmoja
Nemanja Vidic, miaka tisa na miezi mitano
Shinji Kagawa, mwaka mmoja na miezi 11
Patrice Evra, miaka tisa na miezi miwili
Tom Cleverley, mwaka mmoja na miezi saba
Robin van Persie, miaka saba na miezi saba
Chris Smalling, mwaka mmoja na miezi minne
Darren Fletcher, miaka saba na mwezi mmoja
Ben Amos, miezi 11
Anders Lindegaard, miaka sita na miezi 11
Rafael, miezi tisa
Ashley Young, miaka mitano na miezi minane
David de Gea, miezi mitatu
Antonio Valencia, miaka mitano na miezi saba
Danny Welbeck, miezi mitatu
Wayne Rooney, miaka mitano na miezi mitano
Phil Jones, alikuwa hajazaliwa (Alizaliwa Feb 21, 1992)
Nani, miaka minne na miezi minne
Nick Powell, alikuwa hajazaliwa (Alizaliwa Machi 23,1994)
Jonny Evans, miaka minne na miezi miwili

IDADI YA MECHI NA TIMU ALIZOCHEZEA GIGGS
Manchester United: Mechi 931
Wales: Mechi 64
Timu ya GB: Mechi 4
Jumla: Mechi 999

WACHEZAJI WALIOWEKA REKODI YA KUCHEZA MECHI 1,000 ENGLAND
Peter Shilton
Ray Clemence
Pat Jennings
David Seaman
Tony Ford
Graham Alexander

No comments:

Post a Comment