KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

CHRIS: RIHANA ANANIPENDA, AMENISAMEHE



LOS ANGELES, Marekani
MWANAMUZIKI Chris Brown amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu kitendo chake cha kumpiga na kumjeruhi mpenzi wake, Rihanna na kusema kwamba anakijutia.

Brown alisema mjini hapa wiki hii kuwa, kitendo hicho ni cha kwanza kikubwa kukijutia katika maisha yake.

Japokuwa mwanamuziki huyo wa Marekani amekielezea kitendo hicho kuwa ni makosa, pia amekiri kwamba wameamua kuendelea na uhusiano wao baada ya Rihanna kuamua kumsamehe.

Brown, ambaye anajaribu kubadili mwonekano wake kwa jamii, alisema kwa sasa ameamua kuufanyiakazi uamuzi wa Rihanna kumsamehe.

"Niliujutia usiku ule katika maisha yangu. Lilikuwa kosa kubwa,"alisema mwanamuziki huyo nyota wa miondoko ya R&B.

"Lakini ananipenda, nisemeje? Nimesamehewa, ndio, naufanyiakazi uamuzi wake huo,"aliongeza mwanamuziki huyo.

Brown alisema wameamua kulisahau tukio hilo hata kama watu wengine hawataki kufanya hivyo.

Mwanamuziki huyo alikiri kuwa, baadhi ya wakati hutokea mtu kugombana na mpenzi wake na baadaye kusameheana.

Brown alidaiwa kumpiga na kumjeruhi Rihanna 2009 baada ya kutokea mabishano kati yao.

Kutokana na kukiri kufanya kitendo hicho, mahakama ilimweka mwanamuziki huyo chini ya uangalizi kwa miaka mitano na kutakiwa kufanyakazi za kijamii kwa miezi sita.

Licha ya kuamua kusameheana na kuendeleza uhusiano wao, Brown na Rihanna wamekuwa wakikumbana na upinzani mkali kutoka kwa wanaharakati.

Wapenzi hao wawili wiki iliyopita walisherehekea Rihanna kutimiza miaka 25 katika ufukwe wa Hawaii.

No comments:

Post a Comment