KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

DEFOE APATA MTOTO



LONDON, England
MWANASOKA Jermain Defoe wa klabu ya Tottenham ya England, amepata mtoto wa kwanza baada ya rafiki yake wa zamani wa kike, Anne-Marie Moore kujifungua.

Anne-Marie alijifungua mtoto huyo wa kike wiki iliyopita na kubatizwa jina la Joshua-James Defoe.

Defoe (30) aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kwa muda mfupi na Anne-Marie mwaka jana baada ya kutengana na mpenzi wake wa zamani, Alexandra Burke

Beki huyo alikuwepo hospitali wakati mpenzi wake huyo wa zamani akijifungua na tangu wakati huo amekuwa akimtembelea mwanaye kila siku.

"Defoe amepatwa na furaha ya ajabu kutokana na kuwa baba. Ni tukio linalomfanya mtu apevuke kimaisha na sasa anajiandaa kwa majukumu ya kifamilia,"alisema mtu mmoja wa karibu wa mwanasoka huyo.

Wapenzi hao wawili walifichua kuwa, walitarajia kupata mtoto wa kiume miezi kadhaa iliyopita baada ya penzi lao kuvunjika 2012.

Defoe alipigwa chini na Alexandra, ambaye ni mwanamuziki Mei mwaka jana baada ya kugundulika alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Anne-Marie.

Baada ya fumanizi hilo, Defoe aliamua kuanzisha rasmi uhusiano wa kimapenzi na Anne-Marie.

Licha ya wapenzi hao wawili kutoishi pamoja kwa sasa, Defoe alikuwepo karibu ya Anne-Marie wakati wa kujifungua.

Anne-Marie (32) alifichua kuwa ana uja uzito wakati alipotuma picha ya x-ray ikionyesha tumbo lake kwenye mtandao wa Facebook.

Rafiki mmoja wa Anne-Marie alidokeza kuwa, wapenzi hao wawili walikuwa pamoja kwa muda mwingi kabla ya kila mmoja wao kuamua kuishi kivyakevyake.

Defoe amewahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na nyota kadhaa wa muziki na filamu, wakiwemo Imogen Thomas, Chantelle Houghton na Danielle Lloyd.

Lakini baada ya kupata mtoto, watu wake wa karibu wamesema, maisha ya ujana aliyokuwa nayo Defoe kwa sasa yamefikia ukingoni.

No comments:

Post a Comment