KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

JANET JACKSON AFUNGA NDOA KWA SIRI


LOS ANGELES, Marekani
MWANAMUZIKI nyota wa Marekani, Janet Jackson ameibuka na kusema kuwa, alifunga ndoa na rafiki yake, mfanyabiashara wa Qatar tangu mwaka jana.

Janet (46), ambaye ni ndugu wa mwanamuziki nyota wa zamani wa miondoko ya pop duniani, marehemu Michael Jackson, alifunga ndoa na mfanyabiashara huyo, Wissa Al Mana (37) kwa siri.

Mwanadada huyo ameamua kuanika ukweli huo hadharani ili kukanusha taarifa zilizokuwa zikiripotiwa na vyombo vya habari kuhusu ndoa hiyo.

Kwa mujibu wa Janet, waliamua kuifanya ndoa hiyo iwe siri ili kuepuka taarifa potofu zinazoweza kutolewa na vyombo vya habari.

"Uvumi uliozagaa kuhusu ndoa yetu sio wa kweli. Tulifunga ndoa mwaka jana katika harusi ndogo, nzuri na iliyofanyika kwa siri," ilisema taarifa iliyotolewa kwa pamoja na Janet na Al Mana wiki hii.

Janet amekuwa akifahamika kutokana na kuyafanya maisha yake kuwa siri ili kuepuka kupakaziwa na vyombo vya habari.

Mwanamama huyo amewahi kufunga ndoa mara mbili, lakini ndoa ya kwanza ilivunjika baada ya mwaka mmoja na ya pili ilivunjika baada ya miaka tisa.

Alifunga ndoa kwa mara ya kwanza 1984 na James DeBarge kabla ya kuolewa kwa mara ya pili na Rene Elizondoa 1991.

No comments:

Post a Comment