KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

SIKIA HII KALI YA GUARDIOLA


MADRID, Hispania
KOCHA Mkuu wa zamani wa Barcelona ya Hispania, Pep Guardiola alikuwa akikodi wapelelezi wa kujitegemea kwa ajili ya kufuatilia maisha ya wanasoka wake nyota.

Uamuzi huo wa Guardiola ulilenga kuwaepusha nyota hao wasijihusishe na vitendo vinavyoweza kushusha viwango vyao.

Miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakifuatiliwa na kocha huyo ni Ronaldinho Gaucho, Deco Souza, Samuel Eto’o na Gerard Pique.

Imeelezwa kuwa, Guardiola alianza kufanya hivyo tangu 2008 alipoanza kuinoa timu hiyo hadi alipomaliza mkataba wake mwaka jana.

Chanzo cha habari kimeeleza kuwa, hiyo ndiyo siri kubwa ya mafanikio iliyoyapata Barcelona katika kipindi cha miaka minne ilichokuwa ikinolewa na kocha huyo.

Guardiola (42) aliiwezesha Barcelona kushinda mataji 12 katika miaka minne ya utawala wake, yakiwemo mataji mawili ya ligi ya mabingwa wa Ulaya.

Kwa sasa, Guardiona anajiandaa kuifundisha Bayern Munich ya Ujerumani, akichukua nafasi ya kocha wa sasa wa timu hiyo, Jupp Heynckes. Anatarajia kuanza kazi hiyo mwishoni mwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment