KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 28, 2013

RONALDO: KUIFUNGA BARCELONA RAHAAA



MADRID, Hispania
MSHAMBULIAJI Cristiano Ronaldo wa Real Madrid amesema huwa anajisikia raha timu yake inapoifunga Barcelona katika michuano mbalimbali.

Ronaldo alisema hayo juzi baada ya Real Madrid kuichapa Barcelona mabao 3-1 na kufuzu kucheza fainali ya michuano ya Kombe la Del Rey kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-2.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nou Camp, Ronaldo aliifungia Real Madrid mabao mawili kati ya matatu. Bao lingine lingine lilifungwa na Raphael Varane.

"Inafurahisha, nitakuwemo kwenye vitabu vya kumbukumbu ya soka ya Hispania,"alisema mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ureno.

Ronaldo alisema wamekuwa wakipata matokeo mazuri kila wanapocheza na Barcelona kwenye uwanja wa Nou Camp kuliko wanavyocheza nao Santiago Bernabeu.

"Ulikuwa mchezo nzuri. Tulicheza vizuri sana. Kuanzia dakika ya kwanza hadi ya mwisho, tulicheza kwa ari kubwa. Tulicheza vizuri kuliko Barcelona. Kufunga mabao matatu kwenye uwanja wa Nou Camp ni kazi ngumu,"alisema.

Ronaldo alisema kwa sasa, michuano ya ligi ya Hispania haina umuhimu kwao kutokana na kuwa nyuma kwa tofauti na pointi nyingi kati yao na Barcelona.

Alisema wameamua kuelekeza akili zao katika michuano ya Del Rey na ligi ya mabingwa wa Ulaya kwa vile wana uwezo wa kufanya vizuri.

No comments:

Post a Comment