KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, April 30, 2010

WAMBURA: Nitapigania haki yangu hadi mwisho

MGOMBEA nafasi ya mwenyekiti katika uchaguzi mkuu wa Simba, Michael Wambura ambaye ameenguliwa kwenye kinyang'anyiro hicho, ameapa kupigana kufa na kupona kutetea haki yake.
Akizungumza muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka (TFF), Deogratias Lyatto, kutangaza matokeo ya pingamizi zilizowekwa kwa wagombea.
Wambura alisema anasubiri kupatiwa nakala ya uamuzi wa kuenguliwa kwake, na baada ya hapo atachukua hatua.
"Binafsi sishangazwi na taarifa ambazo zimetolewa leo (jana) na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Lyatto. Kwani kilichokuwa kikiandikwa na vyombo vya habari ndicho hicho kilichotokea," alisema.
Alisema anawasiliana na wanacheria wake kuona nini cha kufanya, ili kumwezesha kuitetea haki yake ambayo inaonekana dhahiri kupokwa na baadhi ya watu kwa maslahi yao binafsi.
Wambura ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa kilichokuwa Chama cha Soka Tanzania (FAT) (sasa Shirikisho la Soka nchini (TFF), alisema tangu mchakato wa upitiaji wa majina ya wagombea ulipoanza katika kamati ya uchaguzi ya Simba alijua kuweko mizengwe.
Alisema kuna watu (hakuwataja majina) ambao walikuwa wakifanya mbinu chafu, ikiwa pamoja na kutumia kiasi kubwa cha fedha ili kumchafua, asipate tiketi ya kuingia kwenye uchaguzi huo.
"Pamoja na kuwa kanuni za uchaguzi zineelekeza tunaweza kukata rufani kwa Kamati ya Rufani ya TFF, sitasema hivyo kwanza. Nasubiri nipate hiyo nakala na kisha nitazungumza na wanasheria wangu," alisema.
Wambura alisema wanasheria wake ndio watakuwa na jukumu la kumweleza nini anapaswa kukifanya, baada ya kutangazwa kuengeliwa kwenye mchakato huo.
"Kuna kipengele cha 'Integrity' (kukosa uaminifu) ambacho mara kwa mara wamekuwa wakikitumia juu yangu, lakini nataka wanielezee zaidi kuhusiana na kitu hicho ambacho kinanichafua mara zote," alisema.
Akijibu swali kama ana mpango wa kulipeleka suala hilo mahakamani, alisema ni mapema mno kwake kuzungumzia jambo hilo.
"Siwezi kuzungumzia suala la kwenda mahakamanin sasa, kwani kulingana na kanuni ya uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ibara ya 12, inaelekeza mgombea kufuata taratibu na kukata rufani kwa Kamati ya Rufaa, kama ikishindikana baadaye Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo," alisema.
Kuenguliwa kwa Wambura, Zacharia Hans Poppe na Hassan Dalali kwenye nafasi hiyo kumeifanya nafasi hiyo isaliwe na wagombea watatu, ambao ni Hassan Othman'Hassanoo', Andrew Tupa na Ismail Aden Rage.

No comments:

Post a Comment