KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, April 29, 2010

Miss Utalii Vyuo Vikuu leo Arusha

MWANAMUZIKI machachari nchini, Ndanda Kosovo anatarajiwa kutoa burudani wakati wa shindano la Miss Utalii Vyuo Vikuu Kanda ya Kaskazini, linalotarajiwa kufanyika leo.
Mratibu wa shindano hilo, Upendo Simwita alisema juzi kuwa, warembo 12 kutoka vyuo mbalimbali vya elimu ya juu katika kanda hiyo, wanatarajiwa kuwania taji hilo.
Upendo alisema shindano hilo limepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Naura Springs ya mjini Arusha.
Mbali na Kosovo, mratibu huyo alisema, shindano hilo pia litapambwa kwa burudani ya muziki wa kizazi kipya kutoka kwa msanii Belle 9 kutoka mjini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Upendo, washindi watatu wa kwanza wa shindano hilo watashiriki katika fainali ya Taifa iliyopangwa kufanyika Julai mwaka huu mjini Dar es Salaam.
Alisema washiriki katika shindano hilo watachuana katika mavazi ya ubunifu, utalii na kutokea matembezini nyakati za jioni. Pia alisema watachuana katika shindano la vipaji, ambapo watashindanishwa kuimba na kucheza ngoma za kiasili.
Upendo amewataka wakazi wa mji wa Arusha kujitokeza kwa wingi kushuhudia shindani hilo, ambalo lengo lake kubwa ni kutangaza vivutio vya kitalii vilivyopo nchini.

No comments:

Post a Comment