KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, April 19, 2010

FID Q: Ilinichukua mwaka kurekodi na Bi Kidude





MSANII Khalid Kubanda ‘Fid Q’ amesema ilimchukua mwaka mmoja kukamilisha kazi ya kurekodi wimbo wake mpya wa ‘Juhudi za wasiojiweza’.


Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Fid Q alisema alichelewa kukamilisha kazi hiyo kutokana na mazingira magumu ya kumpata mkongwe wa taarab nchini, Fatuma binti Baraka ‘Bi Kidude’.


Fid Q alirekodi wimbo huo kwa kumshirikisha Bi Kidude, ambaye sauti yake imeufanya uwe wenye mvuto na mahadhi ya aina yake.


“Kikwazo kilikuwa Bi Kidude, ambaye kila nilipomfuata Zanzibar tulikuwa tukipishana,”alisema msanii huyo.


“Siku tuliyofanikiwa kufanyakazi hiyo, nilipanda ndege hadi Zanzibar, lakini pamoja na kufika mapema, nilifanikiwa kukutana naye nyakati za usiku,”aliongeza.


Fid Q alisema walirekodi wimbo huo nyakati za usiku katika studio za Jupiter zilizopo Zanzibar na kuikamilisha kwa siku moja.


“Pamoja na kukaa na Bi Kidude studio kwa saa kadhaa, kesho yake tulipokutana na kumsalimia,
alishindwa kunikumbuka. Akaniuliza wewe nani?” Alisema.


Msanii huyo alisema hakushangaa kuulizwa swali hilo na Bi Kidude kwa vile umri wake ni mkubwa na hana kumbukumbu nzuri. Bi Kidude anakadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 100.


Kibao cha ‘Juhudi za wasiojiweza’ na vinginevyo vya msanii huyo vinapatikana katika albamu yake mpya, inayokwenda kwa jina la ‘Propaganda’.

No comments:

Post a Comment