KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 25, 2012

WAPINZANI WA NGORONGORO WATUA DAR

TIMU ya soka ya Taifa ya vijana wa chini ya umri wa miaka 20 ya
Nigeria (Flying Eagles) ilitarajiwa kuwasili nchini jana kwa ajili ya
pambano lake la michuano ya Afrika dhidi ya timu ya vijana wa
umri huo ya Tanzania, Ngorongoro Heroes.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface
Wambura alisema jana kuwa, timu hiyo ilitarajiwa kuwasili saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir ikiwa na msafara wa watu 30,
wakiwemo wachezaji 18.
Flying Eagles itapambana na Ngorongoro Heroes katika mechi ya
kwanza ya raundi ya pili itakayofanyika Jumapili kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam. Mechi hiyo imepangwa kuanza saa 10
jioni.
Mechi hiyo ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za 18 za Afrika kwa
vijana wenye umri chini ya miaka 20 zitakazochezwa mwakani
nchini Algeria, itachezeshwa na waamuzi kutoka Kenya wakati
kamishna ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Flying Eagles inayofundishwa na kocha John Obuh juzi ilicheza
mechi ya kirafiki na Rwanda (Young Amavubi) kwenye Uwanja wa
Amahoro jijini Kigali. Nigeria ililala bao 1-0.
Msafara wa timu hiyo unaongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya
Ufundi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Nigeria (NFF), Chris
Green.
Baadhi ya wachezaji waliomo katika kikosi cha Flying Eagles ni
Chidi Osuchukwu, Alhaji Gero, Shehu Abdullahi, Aminu Umar,
Aliyu Mohamed, Uche Agbo, Jonah Usman, Harrison Egbune,
Hassan Abubakar na Yahya Adamu.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya rangi ya
chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C itakuwa sh. 5,000.
Kiingilio kwa VIP A itakuwa sh. 10,000.

No comments:

Post a Comment