KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 25, 2012

Breaking News!!! Issa Kihange afariki dunia

KIUNGO wa zamani wa timu ya soka ya Simba, Issa Kihange amefariki dunia.
Kihange alifariki dunia juzi maeneo ya nyumbani kwake, Mbezi Jogoo, Dar es Salaam baada ya kuanguka uwanjani wakati akicheza mechi za maveterani.
Mtandao wa Bin Zubeiry umemkariri kiungo wa zamani wa Yanga, Waziri Mahadhi ‘Mandieta’ aliyekuwapo maeneo ya tukio akisema kuwa, Kihange alinguka wakati akishangilia bao alilofunga.
Kwa mujibu wa Mahadhi, mara baada ya kuanguka, mwanasoka huyo wa zamani alikimbizwa katika hospitali ya IMTU, ambako mauti yalimfika.
Kihange alikuwemo kwenye kikosi cha Simba kilichotwaa taji la pili la michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati mwaka 1991 mjini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment