KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 31, 2012

AZIM DEWJI AIPONGEZA YANGA

MWANACHAMA maarufu wa klabu ya Simba, Azim Dewji ameipongeza timu yasoka
ya Yanga kwa kufanikiwa kutetea ubingwa wa michuano ya AfrikaMashariki na Kati.Yanga ilifanya hivyo mwishoni mwa wiki, baada ya kuizamisha Azam kwamabao 2-0 katika mchezo mkali wa fainali kwenye Uwanja wa Taifa, Dares Salaam.

Akizungumza jana, Dewji aliyewahi kuifadhili Simba na kuifikisha fainali za Kombe la CAF mwaka 1993, alisema pamoja na yeye kuwa `SimbaDamu’, ana kila sababu za kuimwagia sifa Yanga kwa kuwa imezika harakamatatizo yake na kugeukia kusaka maendeleo.

“Huwezi kuamini kama Yanga iliyopigwa 5-0 na kuibua tafrani nzitoJangwani, ndiyo hii ya leo. Wameikubali hali na kubadilika ndani ya muda mfupi sana. Wana amani na matunda yake yameonekana ingawa walikuwa na kipindi kifupi cha kusuka timu na kurejesha mshikamanondani ya klabu.

“Naipongeza Yanga na hasa Mwenyekiti wake, Yussuf Manji kwa sababunaamini imani ya
wanachama juu yake ndiyo iliyorekebisha hali haraka,naye kama kiongozi kuhakikisha usajili makini unafanyika, kochaanapatikana na uzalendo ndani ya Yanga unarejea,” alisema Dewji.

Aliongeza kuwa, pamoja na matunda ya haraka ya uongozi wa Manji,wana-Yanga wanapaswa kumpa ushirikiano ili kuiondoa Yanga katikautegemezi wa miaka nenda rudi, huku akisisitiza Manji hatabaki Yangamilele.

“Wana kiongozi shupavu, sasa washirikiane naye kuujenga uchumi waklabu. Haya mambo
ya kutegemea mtu kila kukicha si mazuri. Na hili sikwa Yanga tu, hata Simba na klabu nyingine
zinapaswa kujikita katikakujijenga kiuchumi ili ziwe na jeuri ya fedha bila ya kutegemea mifukoya mwanachama mmoja mmoja,” alisema.

Akisisitiza kujijenga kiuchumi, Dewji mmoja wa wafanyabiashara maarufunchini, alisema viongozi wa klabu kubwa za Simba na Yanga zianzekuutumia mtaji wa wanachama kujijenga, huku akitolea mfano kuwa, kilamoja ina zaidi ya wafuasi milioni 15, lakini klabu zinabaki kuwamasikini.

“Huu ni mtaji mkubwa sana, lakini utashangaa klabu haina hata asilimia moja (150,000) ya wanachama wa kweli. Kila siku utasikia wanachama3,000 hadi 6,000. Kiongozi wa klabu anachaguliwa na wanachamawasiofika 2,000?

“Jamani, kwa klabu inayoshabikiwa na mamilioni ya watu inashindwajekujijenga kiuchumi kwa kuwatumia mashabiki wake waliozagaa kila konaya nchi? Jiulize, kama angalau hao watu 150,000 tu wakilipa ada yamwaka ya 12,000 ambayo hata hivyo bado ni ndogo, si wanaweza kuvuna shbilioni 1.8 kwa mwaka, hizi si fedha nyingi?

“Kuna haja ya kufanya mapinduzi ya kweli, badala ya kufikiria kuifungaSimba au Yanga na kutwaa ubingwa wa Bara. Timu yenye uchumi imara,ndiyo inayokuwa na jeuri ya kuwa na kikosi imara na hivyo kufanyavizuri zaidi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. Huko ndikotunakopaswa kwenda,” alisisitiza.

No comments:

Post a Comment