KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, July 15, 2012

Simba yavutwa sharubu na URA



MABINGWA wa soka wa Tanzania Bara, Simba jana walianza vibaya michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuchapwa mabao 2-0 na URA ya Uganda katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kipigo hicho cha Simba kimekuja siku moja baada ya watani wao wa jadi, Yanga nao kukubali kipigo hicho cha mabao kutoka kwa Atletico ya Burundi.

Mshambuliaji Fenni Ali ndiye aliyewanyong'onyesha mashabiki wa Simba wa Simba baada ya kuifungia mabao hayo mawili, moja katika kila kipindi.

Katika mechi zingine za michuano hiyo zilizochezwa jana, Azam ililazimishwa kutoka sare ya bao 1-1 na Mafunzo ya Zanzibar kwenye uwanja wa Chamazi wakati AS Vita iliitandika Ports ya Djibouti mabao 7-0.

No comments:

Post a Comment