KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 25, 2012

MAKAMBA AMJIBU ZITTO KUHUSU ON MOBILE

NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia jana alimuumbua mbunge wa Kigoma Kaskazini Zuberi Zitto kuwa serikali ilishaisimamisha kampuni ya Onmobile kuendelea kufanya kazi toka mwezi Juni mwka huu.
Alisema serikali iliamua kuisimamisha kampuni hiyo kuendelea kufanya kazi baada ya kampuni hiyo kuandika barua ya kuomba leseni.
Makamba alisema baada ya serikali kuipokea barua hiyo tarehe 29 february mwaka huu iliijibu barua hiyobaada ya kubaini mapungufu mbalimbali katika maombi hayo.
Naibu huyo alisema baadhi ya mapungufu hayo ni pamoja na kampuni hiyo kutosajiliwa BRELA na kutoa mchanganuo wa kibishara.
Hata hivyo, alisema baada ya serikali kugundua kuwa pamoja na kuomba leseni pia kampuni hiyo ilikuwa ikiendelea kufanya kazi kupitia kampuni za Vodacom na Airtel
Alisema hivyo hoja iliyotolewa na Zitto kuwa kampuni hiyo inafanya kazi bila leseni ilishagunduliwa na serikali na kuchukuliwa kwa hatua.
Akizungumzia kuhusiana na wizi wa kazi za wasanii, Makamba alisema serikali haitakubali kuona wasanii hao wanaibiwa kazi zao.
Alisema vita dhidi ya wizi wa kazi hizo ilianza toka mika ya 2009 ambako Rais Jakaya Kikwete alitoa jumla ya sh .milioni 16 kutoka kwenye mfuko wa Rais kwa ajili ya kumlipa mshauri mwelekezi kushauri TRA kuweka stika katika kazi za wasanii hao.
Naibu huyo alisema kabla ya kuondoka katika Ofisi ya Rais, yeye ndiye aliyetumwa na Rais kwenda kuonana na watalaamu mbalimbali ili kuangalia uwezekano wa kusaidia wasanii hao.
“Hivyo vita hii ilianza na Mheshimiwa Rais Mwenyewe na alinituma mimi nikaenda sehemu mbalimbali na tulifanya vikao na wasanii nikiwa mwenyekiti kujadiri maslahi yao’’
“Pia Rais Kikwete ndiye Rais wa kwanza ambaye aliwashirikisha wasanii wa Bongo Fleva na hata katika kampeni zake za uchaguzi Mkuu wa Rais mwka 2009’’
Makamba alisema ni haki ya msanii kulipwa mrahaba kwa kila wimbo wake unapotumiwa na kamapuni ya simu au hata redio.
Alisema serikali itaendelea kuwapigania wasanii hao pale makampuni ya simu yanapotumia nyimbo zao kwani ni haki yao.

No comments:

Post a Comment