KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 10, 2012

Temeke yatinga nusu fainali Copa Coca Cola

Temeke imekuwa timu ya kwanza kupata tiketi ya kucheza nusu fainali kwenye michuano ya mwaka huu ya Copa Coca-Cola baada ya kuing’oa Mjini Magharibi kwa mikwaju ya penalti.
Mechi hiyo ya kwanza ya robo fainali imechezwa leo asubuhi (Julai 10 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ambapo hadi dakika 90 za kawaida zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.
Mjini Magharibi ndiyo walioanza kupata bao dakika ya 79 lililofungwa na Salum Maulid wakati Abdul Hassan aliisawazishia Temeke dakika ya 90.
Waliofunga penalti kwa upande wa Temeke ni Baraka Ntalukundo, Khalid Mwendakamo, Mohamed Dikougwa na Abdul Hassan wakati aliyekosa ni Anwar Kilemile. Waliokosa kwa Mjini Magharibi ni Abdulrahman Mohamed na Salum Maulid wakati waliofunga ni Alawi Kombo na Salum Shukuru.
Katika nusu fainali, Temeke itacheza na mshindi wa mechi ya robo fainali kati ya Kinondoni na Mwanza itakayochezwa kesho asubuhi (Julai 11 mwaka huu) Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Robo fainali ya pili ya michuano hiyo kati ya Mara na Morogoro ilitarajiwa kuchezwa leo jioni kwenye uwanja huo huo. Mechi nyingine ya robo fainali itakayowakutanisha Dodoma na Tanga itachezwa kesho jioni.

No comments:

Post a Comment