KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 24, 2012

Simba yatupwa nje Kombe la Kagame, yapigwa 3-1 na Azam

SIMBA leo imetolewa katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Azam katika mechi ya robo fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mshambuliaji John Bocco ndiye aliyeibuka shujaa wa Azam baada ya kuifungia mabao yote matatu, moja kipindi cha kwanza na mengine kipindi cha pili. Bao pekee la Simba lilifungwa na Shomari Kapombe.

Ushindi huo umeiwezesha Azam kutinga nusu fainali, ambapo sasa itakutana na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Vita imefuzu kucheza hatua hiyo baada ya kuitoa Atletico ya Burundi mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa kuanzia saa nane mchana.

Mechi nyingine ya nusu fainali itazikutanisha Yanga na APR ya Rwanda. Yanga imetinga hatua hiyo baada ya kuitoa Mafunzo ya Zanzibar kwa penati 5-3 wakati APR iliitoa URA ya Uganda kwa mabao 2-1.

Kwa mujibu wa ratiba, mechi zote mbili za nusu fainali zitachezwa Alhamisi wiki hii. Mechi ya kwanza itazikutanisha Azam na APR wakati katika mechi ya pili, Yanga itavaana na AS Vita.

Fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kupigwa Jumapili, ikitanguliwa na mechi ya kutafuta mshindi wa tatu.

No comments:

Post a Comment