KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, July 30, 2012

AIRTEL TANZANIA YAENDELEA KUSAMBAZA MAWASILIANO KANDA YA ZIWA

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh Charles Kitwanga akikata utepe kuashira uzinduzi wa mawasiliano uliojengwa na Airtel Tanzania, nje kidogo ya mkoa wa Mwanza katika wilaya ya Misungwi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma zake zote kama intaneti, Airtel Money na kupiga simu vijiji vya Nyamainza, Buhunda, Ishoke na Seke. Wengine, wa kwanza kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando. Hafla ya uzinduzi wa mnara huu ilifanyika katika kijiji cha Nyamayinza wilayani Misungwi mwishoni mwa wiki



KAMPUNI ya Airtel Tanzania, imezindua mwishoni mwa wiki imezindua mtambo kabambe wa mawasilano katika mkoa wa kanda ya Ziwa nje kidogo ya mkoa waMwanza katika wilaya ya Misungwi, ikiwa ni mkakati wa kampuni hiyo kuendelea kufikisha huduma zao bora vijijini.

Akizindua mnara huo mpya, Naibu Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh, Charles Kitwanga ‘Mawe Matatu’, alisema Maendeleo vijijini yatakuwakwa kasi sana iwapo wananchi watatumia mawasiliano ya simu za mkononi kutafuta masoko ya madini, mifugo au vyakula anavyozalisha sehemu mbalimbali.

Waziri Kitwanga alibainisha hayo katika kijiji cha Nyamayinza, kata ya Gulumungu wilaya ya Misugwi Mkoani Mwanza wakati akiongea na wananchi na kuzindua mnara wa mawasiliano uliojengwa na kampuni ya Airtel Tanzania.

“Mawasiliano yana faida kubwa sana duniani na ndio hufanya maendeleo ya jamii kwenda kwa kasi, hivyo wananchi wa vijiji vyote vinavyoizunguka Nyamayinza, tumieni fursa ya kupata mawasiliano haya ya Airtel kwa kuendesha au kuendeleza biashara zenu, pia anzisheni biashara za kutuma na kupokea pesa za Airtel Money na mtumie mawasiliano haya haya pia kutafuta wateja wa kutosha katika bidhaa za kilimo na mifugo mnazozalisha,”alisema.

Nae Meneja Mauzo wa Airtel Kanda ya Ziwa Bw, Garlus Mgawe, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Airtel Tanzania, alisema; “Airtel kwa kukamilisha dhamira yetu ya kutoa mawasiliano yenye uhakika kwa mwaka huu, tunaanza na kuzindua mtambo huu wa mawasiliano hapa wilayani Misungwi, utakaowezesha zaidi ya watu 15,000 waliopo vijiji vya Nyamainza, Buhunda, Ishokela, na Seke kuwasiliana na ndugu na jamaakwa uhakika wakiwa Airtel,”alisema.

Kupatikana kwa mtandao huu wa Airtel, pia kutasaidia wakazi wa vijiji vyote na jirani kufurahia huduma zote za Airtel ikiwemo ile ya Airtel Money, kutuma na kupokea sms, pamoja na kufurahia mtandao bora na nafuu wa Intaneti.

Uboreshwaji na uwekaji wa Minara ya mawasiliano ya Airtel katika vijiji, unawezeshwa kwa ushirikiano na Serikali na Mamlaka za Mawasiliano nchini kwa kuwa imeweka mikakati bora zaidi wakati wa uwekaji wa miundo mbinu hiyo ya mawasiliano kila mahali.

Akiongezea kuhusiana na mpango wa kusambaza mtandao unaoendelea, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Bw Jackson Mmbando alisema; “Kuongezeka kwa mahitaji ya huduma za mawasiliano kutokana na mazingira au kupanuka kwa shughuli za jamii, ndio kunatufanya (Airtel Tanzania) kuitikia wito wa kutanua zaidi wigo wa mtandao wetu kwa maeneo yote.

“Huduma ya mawasiliano imekuwa moja kati ya nyenzo muhimu katika kuwezesha shughuli nyingi za kijamii nchini Tanzania na duniani kote, kupanuka na kufikisha mawasiliano vijijini ni chachu ya kukua kwa uchumi na kuwezesha jamii iliyopo maeneo hayo kupata miundombinu mbadala katika shughuli za uzalishaji.

Airtel bado tunategemea kuendelea kupata ushirikiano wa kutosha kati yetu na serikali katika kuhakikisha tunafikisha mawasiliano vijijini, kwa kutuwekea mfumo bora wa kulipa kodi na kupata vibali vya kuweka mitambo ya mawasiliano ili kufaidisha jamii,”alisema.

Airtel ni mtandao bora ulioenea zaidi na kutoa mawasiliano nchini kote, kwa kufikisha mawasiliano ya uhakikia kwa takribani asilimia 85, kwenye maeneo ya miji na vijiji nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment