KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 25, 2012

MR. NICE SASA AGEUKIA TAARAB

BAADA ya ukimya wa muda mrefu, msanii machachari wa muziki wa kizazi kipya nchini, Lucas Nkenda amesema anajiandaa kupakua albamu yake mpya ya miondoko ya mduara.
Nkenda, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Mr. Nice, alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, albamu yake hiyo itajulikana kwa jina la Tabia gani.
Alisema ameamua kubadili mahadhi ya muziki anaopiga kutokana na maombi ya mashabiki wake wengi, hasa waliopo katika mikoa ya kanda ya Ziwa.
Msanii huyo aliyetamba vilivyo mwanzoni mwa miaka ya 2000 alisema, amefurahishwa na mapokezi makubwa aliyoyapata wakati wa ziara yake katika mikoa hiyo hivi karibuni.
“Sikutegemea kupata mapokezi makubwa kiasi kile. Kusema kweli nimefurahishwa kuona kwamba mashabiki wangu wa ndani na nje ya nchi bado wananikubali sana,”alisema.
Kwa mujibu wa Mr. Nice, anatarajia kuizindua albamu yake hiyo mara baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Katika hatua nyingine, msanii Fred Maliki ‘Mkoloni’ ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Nilivyo na Walivyo.
Mkoloni alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, kibao hicho kinaelezea matatizo mbali mbali yanayowakumba wananchi wa Tanzania.
Akifafanua, Mkoloni alisema kibao hicho kinaelezea hali duni za maisha, ambazo kwa kiasi kikubwa zinasababishwa na baadhi ya viongozi wa serikali kuweka mbele zaidi maslahi yao binafsi.

No comments:

Post a Comment