KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, July 31, 2012

JB AMGALAGAZA RAY

Msanii nyota wa filamu, Jacob Steven, maarufu kwa jina la JB

Msanii machachari wa bongo movie, Vicent Kigosi, maarufu kwa jina la Ray


Mcheza filamu nyota nchini, Jacob Steven ameibuka mshindi wa shindano la mcheza filamu bora wa kiume wa bongo lililoandaliwa na blogu ya liwazo zito.

Shindano hilo liliwashirikisha wacheza filamu wanne wa kiume wa bongo movie na washiriki walipigiwa kura na wasomaji wa blogu hii kutoka sehemu mbali mbali duniani.

Jacob, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la JB aliibuka mshindi baada ya kupata kura 33, ambazo ni sawa na asilimia 82 ya kura zilizopigwa.

Vicent Kigosi, maarufu kwa jina la Ray alishika nafasi ya pili baada ya kupata kura nne, ambazo ni sawa na asilimia 14,

Single Mtambalike, maarufu kwa jina la Richie alishika nafasi ya tatu baada ya kuambulia kura mbili wakati Issa Mussa, almaarufu kwa jina la Cloud aliambulia kura moja.

Msanii Awadh Mahsen, maarufu kwa jina la Dk. Cheni ndiye pekee, ambaye hakuambulia kura katika washiriki watano walioshindanishwa katika shindano hili.

Mmiliki wa blogu ya liwazo zito, Rashid Zahor amesema lengo la kuandaa shindano la aina hii ni kuwapa nafasi wasanii wa fani mbali mbali wajitambue kupitia kwa watazamaji na mashabiki wa fani wanazoshiriki.

Zahor, maarufu kwa jina la Ramoza alisema kupitia kura hizi zinazopigwa na wasomaji na watazamaji wa fani hizo, wasanii wanaweza kujitambua namna wanavyokubalika ama wasivyokubalika na mashabiki wao na nini wafanye ili waweze kupiga hatua zaidi.

Alimpongeza JB kwa kuibuka mshindi wa shindano hilo na kuwashukuru wasomaji wote wa blogu hii walioshiriki kupiga kura na wale wanaoipitia kila siku kwa ajili ya kupata taarifa mbali mbali zinazohusu michezo na burudani ndani na nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment