KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, July 25, 2012

CECAFA YAWAPONGEZA WAAMUZI WA TWALIPO

BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limewapongeza waamuzi wa kituo cha Jeshi cha Twalipo kwa umakini wao katika kuchezesha soka.
CECAFA ilitoa pongezi hizo wiki hii kupitia Katibu Mkuu wake, Nicholas Musonye wakati wa mahojiano maalumu na Burudani mjini Dar es Salaam.
Musonye alisema uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutoa mafunzo ya uamuzi kwa vijana wa kituo hicho, ambao umri wao ni chini ya miaka 20, unapaswa kuwa mfano wa kuigwa.
Alisema aliwaona vijana hao wakati wa michuano ya Rollingstone iliyofanyika nchini Burundi hivi karibuni na kuvutiwa na uchezeshaji hao.
Waamuzi hao ndio pekee waliochezesha michuano hiyo, kufuatia ombi maalumu la Wizara ya Michezo ya Burundi.
Mbali na michuano hiyo, waamuzi wa kituo hicho pia wamekuwa wakitumika kuchezesha michuano ya Kombe la Uhai na Copa Coca Cola iliyomalizika hivi karibuni mjini Dar es Salaam.
“Nilikuwepo nchini Burundi hivi karibuni kushuhudia mashindano ya Rolling Stone na nilifurahishwa kuona waamuzi watoto kutoka Tanzania ndio waliochezesha mashindano hayo,”alisema.
“Binafsi nawapongeza sana viongozi wa TFF kwa kubuni utaratibu wa kutoa mafunzo ya uamuzi kwa vijana wadogo na ni mfano wa kuigwa wa nchi zingine wanachama wa CECAFA,”aliongeza.
“Nadhani wakati umefika kwa viongozi wa nchi zetu kujitahidi kuboresha viwango vya waamuzi wao na ikiwezekana kuiga mfano wa TFF wa kuwaandaa waamuzi tangu wakiwa vijana kwa lengo la kukuza weledi wao,” alisema Musonye.

No comments:

Post a Comment