KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, November 15, 2012

GENEVIEVE ANG'ARA



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa kike wa Nigeria, Genevieve Nnaji ametajwa kuwa miongoni mwa wanawake 100 wapambanaji na wenye mvuto duniani kutokana na shughuli zao.
Jarida la Arise limemworodhesha Genevieve katika nafasi ya nane miongoni mwa wanawake wenye mvuto duniani katika masuala ya utamaduni, habari na michezo.
Mwandishi wa habari na mwanaharakati, Ahdaf Soueif wa Misri anashika nafasi ya kwanza katika orodha hiyo, akifuatiwa na mwanamuziki Angelique Kidjo wa Benin na mcheza filamu Angelina Jolie mwenye maskani yake nchini Marekani.
Mwanamuziki Buika wa Equatoria Guinea ameshika nafasi ya nne, mwandishi wa habari Charlayne Hunter-Gault wa Marekani ameshika nafasi ya tano, mwigizaji Charlize Theron wa Afrika Kusini ameshika nafasi ya sita wakati mtunzi wa vitabu Chimamanda Ngozi wa Nigeria ameshika nafasi ya saba.
Kwa upande wa siasa na harakati, Katibu Mkuu Msaidizi wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro wa Tanzania ameshika nafasi ya pili, nyuma ya Mkenya, Aicha Bah Diallo, ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya elimu.
Katika orodha hiyo, pia yumo Mtanzania, Elsie Kanza, ambaye ni Mkurugenzi wa World Economic Forum, ambaye ameshika nafasi ya nane.
Kwa upande wa biashara na sheria, Mtanzania Genevieve Sangudi ameshika nafasi ya nane. Sangudi ni Mkurugenzi Mtendaji wa Carlyle Group Africa.
Jarida la Arise linachapishwa nchini Uingereza na kuuzwa katika sehemu mbali mbali duniani.

No comments:

Post a Comment