KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, November 26, 2012

ZANZIBAR HEROES YABANWA, RWANDA YASHINDA



TIMU ya soka ya Zanzibar, Zanzibar Heroes leo imeshindwa kutamba mbele ya Eritrea baada ya kulazimishwa kutoka nayo suluhu katika mechi ya kundi C iliyopigwa kwenye Uwanja wa Namboole mjini Kampala, Uganda.
Katika mechi hiyo, tatizo kubwa la Zanzibar Heroes lilikuwa umaliziaji mbovu wa washambuliaji wake, ambao walishindwa kumalizia mipira ya mwisho.
Katika mechi nyingine ya kundi hilo iliyochezwa leo, Rwanda iliichapa Malawi mabao 2-0.
Matokeo hayo yameiwezesha Rwanda kuongoza kundi hilo ikiwa na pointi tatu baada ya kucheza mechi moja, ikifuatiwa na Eritrea na Zanzibar zenye pointi moja kila moja.
Mabao ya Rwanda yalifungwa na Jean Baptiste Mugiraneza na Haruna Niyonzima dakika ya 37 na 79.

No comments:

Post a Comment