KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 21, 2012

TIKETI KOMBE LA AFRIKA KUUZWA KWA MTANDAO


MASHABIKI wanaotaka kushuhudia fainali za 29 za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazofanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini, watapata tiketi kwa njia ya mtandao.
Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) limeeleza kupitia mtandao wake juzi kuwa, tiketi hizo zitauzwa kupitia mtandao wa www.afcon2013booking@eqtickets.com na pia kupitia simu namba +27 879803000.
Fainali za mashindano hayo zimepangwa kuanza Januari 19 na kumalizika Februari 10, 2013. Mashindano hayo yatazishirikisha timu 16 na yatachezwa katika miji ya Johannesburg, Nelson Mandela Bay, Mbombela, Durban na Rustenburg.
Mechi ya fainali itachezwa Februari 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa Soccer City jijini Johanesburg kuanzia saa mbili usiku kwa saa za Afrika Kusini.
Mechi ya ufunguzi wa fainali hizo itachezwa Januari 19 mwaka huu ambapo wenyeji Afrika Kusini (Bafana Bafana) wataumana na Cape Verde kuanzia saa 12 jioni kwenye Uwanja wa Soccer City.
Angola na Morocco zitacheza mechi ya pili kwenye uwanja huo huo kuanzia saa tatu usiku. Timu zote hizo ni za kundi A.
Mabingwa watetezi Zambia wamepangwa kundi C na wataanza mechi yao ya kwanza Januari 21 mwaka huu dhidi ya Ethiopia kuanzia saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Mbombela. Timu nyingine katika kundi hilo ni Nigeria na Burkina Faso.

No comments:

Post a Comment