KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, November 3, 2012

BRIDGIT NDIYE MISS TANZANIA 2012




Bridgit Alfred mwenye umri wa miaka 18, ametwaa taji la Miss Tanzania 2012 katika shindano lililofanyika jana kwenye ukumbi wa Blue Pearl Hotel, uliopo ndani ya jengo la Ubungo Plaza, Dar es Salaam. Ushindi huo ulimwezesha Bridgit kutoka Kinondoni, Dar es Salaam kuzawadiwa sh. milioni nane na gari, ambalo aina yake na thamani yake vitajulikana baadaye. Euegene Fabian aliibuka kuwa mshindi wa pili na kupewa sh. milioni 6.2 wakati Eddah Sylvester aliibuka kuwa mshindi wa tatu na kupewa sh. milioni nne.

No comments:

Post a Comment