KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, November 9, 2012

NYOTA WA AIRTEL RISING STARS KUJIUNGA NA SERENGETI BOYS

Hivi karibuni timu ya taifa ya Tanzania Chini ya miaka 17 ilimchangua kujiunga na kikosi hicho mchezaji nyota wa Airtel Rising Stars Abdul Suleiman ambaye alichaguliwa kati ya mmoja wa wachezaji bora wakati wa kliniki ya soka Afrika iliofanyika Septemba 2012 mjini Nairobi.
Abdul Suleimani ambaye anacheza kama kiungo ubunifu, ameendelea kuwa kivutio kikubwa na kuvuta hisia za makocha wa soka wakati wa michuano ya Airtel Rising Stars katika ngazi zote kuanzia kikanda, kitaifa na kimataifa.
Kuchaguliwa kwake timu ya taifa kumeenda sambamba na hisia chanya za makocha watatu wa shule ya soka wa Manchester United walizoona juu ya mchezaji huyo ambazo ni nidhamu yake, kudhibiti mpira na ujuzi wake wa kutoa pasi, kumekuwa sababu Abdul alichaguliwa kama mmoja wawachezaji nyota ya juu kati ya watatu( 3) baada ya kliniki. Kliniki ya soka iliendeshwa na Makocha kutoka Manchester united kwa kushirikiana na Airtel Afrika yenye lengo la kuwapatia vijana wachezaji wa soka Afrika uzoefu na mbinu za kuwa mchezaji bora na wa kitaalamu
Abdul Suleiman ni mtoto wa mwisho na wakiume pekee katika familia ya watoto wa Nne ya mzee Suleiman Mshilu. Alionyesha uwezo wake wa soka wakati wa michuano ya Airtel Rising stars 2012 akitokea katika shule ya sekondari Tiravi akishiriki kutoka katika mkoa wa kisoka wa Temeke, Abdul aliibuka kuwa mchezaji bora wakati wa michauano ya Airtel Rising Stars kitaifa na kuchaguliwa kuiwakilisha Tanzania katika michuani ya Airtel Rising Stars Tanzania.
Ingawa Timu ya Tanzania haikufika katika hatu ya finali katika michuano ya Afrika uwezo wakucheza mpira wa mchezaji wa Abdul haukufichika kwani aliweza kutoa pasi zilizowawezesha timu yake kufunga mabao mawili wakati wa michuano hiyo
Akiongea kuhusu Mchezaji huyo Kocha John "Del Piero" William amesema Abdul Sulemani ni mchezaji kiungo anayecheza namba 7 na amekuwa mchezaji bora na kuwezesha timu yake ya temeke kuibuka mabingwa kwa kutoa pasi nzuri kwa wafungaji wake na kumwezesha mshambuliaji wa timu yake, Paulo Balama, kuibuka kuwa Mfungaji Bora wakati wa michuano ya taifa ya ARS 2012
Abdul tayari amejiunga na timu ya taifa kwaajili ya kujiandaa na mechi dhidi ya Msumbiji na Kongo. Hii ni ndoto aliyokuwa nayo na sasa imeanza kutimia, "Nafasi Hii itaniwezesha kuonyesha vipaji yangu kwa wadau wa soka dunia nzima na hatimaye kufikia dhamira na lengo langu la kuwa mchezaji wa kimataifa, naamini kwa kuchaguliwa Kucheza timu ya Taifa ni dhahiri kutafungua milango yangu.” alisema mchezaji huyo nyota. Ndoto yangu ni kucheza katika Ligi ya Kiingereza au Kihispania
Akizungumza kuhusu mafanikio hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Sam Elengahoor, alisema: "Tunasikia fahari kwamba shirikisho la mpira Tanzania tayari limeaona mchango wa mpango wa Airtel Rising stars katika kuvumbua na kuinua vipaji vya vijana kwa ajili ya kujiunga na kucheza katika klabu na timu za taifa. Huu ni ushirikiano sawia kwa wachezaji na mpango huu kambambe wa kuinua vipaji. Wachezaji wengine walioshiriki Airtel Rising Stars mwaka huu wanacheza katika vilabu mbalimbali na mashule ikiwemo Paulo Balama na Denis Richard ambao wanacheza katika klabu ya Simba B. Mwaka jana, Airtel Rising Star ilifungua milango kwa Suleiman Bofu kujiunga timu ya Taifa chini ya miaka 17 ambapo Bofu bado ni mchezaji katika kikosi cha timu ya taifa hadi sasa.
Airtel Rising Stars ni mpango maalumu ulioanzishwa na Airtel mwaka 2011 kwa lengo la kuinua, kugundua na kuendeleza wachezaji wenye vipaji chini ya umri wa miaka 17 'katika makundi yote mawili ya kiume na kike. Mpango huu unaendesha katika nchi 15 barani Afrika ambapo Airtel inaendesha shughuli za kibiashara na mikakati iliyopo ni kupanua na kuongeza nchini nyingi zaidi ambazo Airtel inafanya biashara katika msimu ujao.
Wachezaji wengine wengi wenye vipaji katika bara la Afrika wamepokea wito wa kujiunga na timu za Taifa chini ya miaka 17. Airtel Ghana hivi karibuni imesherehekea mchezaji nyota - Priscilla Okyere ambaye alikuwa nahodha na alifunga bao na kuwawezesha timu ya Ghana wanawake chini ya miaka 17 kutwaa medali ya shaba katika Michuano ya FIFA ya mashinda ya kombe la wanawake chini ya miaka 17 ya duani yaliyohitimisha na kufanyika katika Jamhuri ya Azerbaijan.

No comments:

Post a Comment