KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, November 6, 2012

YANGA SPIDI 120



BAADA ya kuichapa Azam mabao 2-0 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara jana iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga imetwaa uongozi wa ligi kuu na huenda isikamatike tena.
Ushindi wa Yanga umeiwezesha kutwaa uongozi wa ligi hiyo, ikiwa na pointi 26 baada ya kucheza mechi 12, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 23 na Azam yenye pointi 21.
Yanga sasa itamaliza mechi zake za mzunguko wa kwanza kwa kumenyana na Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga wakati Simba itahitimisha ligi hiyo kwa kumenyana na Toto African kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Mabao ya Yanga yalifungwa na Didier Kavumbagu na Hamisi Kiiza, moja katika kila kipindi. Mechi hiyo ilishuhudiwa na mjumbe maalumu wa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), Abedi Pele.
Mara baada ya mechi hiyo, uongozi wa Yanga uliamua kuwazawadia wachezaji wake sh. milioni 15 kwa kuifunga Azam.
Hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Yanga kuitambia Azam msimu huu. Katika mechi ya fainali ya Kombe la Kagame, Yanga iliichapa Azam mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment