KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 28, 2012

JB MPIANA KUANZA MAKAMUZI LEO MWANZA



MWANAMUZIKI JB Mpiana na kundi lake la Wenge Musica (BCBG) kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, anatarajiwa kuanza makamuzi yake leo kwa kufanya onyesho mjini Arusha.
Mkurugenzi wa Kampuni ya QS Muhonda, inayoratibu ziara ya mwanamuziki huyo, Joseph Muhonda alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, JB Mpiana na kundi lake wanatarajiwa kufanya maonyesho matatu nchini.
Muhonda alisema JB Mpiana atafanya onyesho lake la pili kesho kwenye viwanja vya Leaders Club vilivyopo Kinondoni, Dar es Salaam, akishirikiana na bendi ya Mashujaa.
Kwa mujibu wa Muhonda, onyesho hilo litakuwa maalumyu kwa ajili ya kusindikiza uzinduzi wa albamu mpya ya Mashujaa, inayokwenda kwa jina la Risasi Kidole.
Alisema onyesho la tatu la mwanamuziki huyo na kundi lake limepangwa kufanyika Jumapili kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
Kwa upande wake, JB Mpiana aliwaambia waandishi wa habari kwenye hoteli ya Double Tree mjini Dar es Salaam juzi kuwa, amekuja kukonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa Tanzania.
"Nina imani waandaaji wamefanya maandalizi ya kutosha, nimekuja na wanamuziki wangi wote 25, nimekuja na vifaa vyangu vyote ili kuwapa burudani ya kutosha,"alisema mwanamuziki huyo.
JB Mpiana aliwataka mashabiki wa muziki nchini wajiandae kupata uhondo wa nyimbo zake mpya zilizomo kwenye albamu ya Biloko.

No comments:

Post a Comment