KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, June 1, 2012

Mrembo wa Nyamagana kupatikana leo

Cecy

Brenda

Amina

Aisha

Shindano la kumsaka mrembo wa kitongoji cha Nyamagana, atakayeshiriki katika shindano la kumsaka mrembo wa Mwanza anatarajiwa kujulikana leo usiku.

Shindano hilo linalotarajiwa kuwashirikisha warembo kadhaa wa kitongoji hicho, limepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Gold Crest.

Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Stoppers Entertainment ya Mwanza na kutakuwepo na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya, akiwemo Linah na Hafsa Kazinja.

Mshereheshaji mkuu wa shindano hilo atakuwa msanii maarufu wa kundi la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya almaarufu zaidi kwa jina la Masanja Mkandamizaji.

No comments:

Post a Comment