KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 3, 2017

YANGA YAVUNA KAPU LA MAGOLI KWA JAMHURI KOMBE LA MAPINDUZI


YANGA jana ilianza michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kishindo baada ya kuicharaza Jamhuri ya Pemba mabao 6-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa inaongoza kundi B kwa tofauti ya mabao ya kufunga kati yake na Azam, ambayo mapema jioni, iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Zimanimoto.

Katika mechi hiyo iliyokuwa ya upande mmoja, Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 4-0. Wafungaji wa mabao hayo walikuwa Simon Msuva na Donaldo Ngoma, waliofunga mawili kila mmoja.

Bao la tano la Yanga lilifungwa na Thabani Kamusoko kabla ya Juma Mahadhi kuhitimisha karamu ya magoli kwa kufunga bao la sita.

No comments:

Post a Comment