KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 26, 2017

RUFANI YA POLISI DAR DHIDI YA SIMBA YATUPILIWA MBALI



KAMATI ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limekataa kuisikiliza Rufaa ya klabu ya Polisi Dar es Salaam dhidi ya Simba SC, kwa sababu taratibu hazikufuatwa.
Polisi Dar iliikatia rufaa Simba SC kwa kumtumia beki wake, Novaty Lufunga katika mchezo wa kombe la TFF, maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) hatua ya 32 Bora Jumapili, Uwanja wa Uhuru, Dar rs Salaam.
Katika mchezo huo ambao Simba ilishinda 2-0, mabao ya Pastory Athanas kipindi cha kwanza na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ kipindi cha pili, Lufunga alikuwa benchi kama mchezaji wa akiba muda wote mchezo.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas amesema kwamba Rufaa ya Polisi haikusikilizwa kabisa kwa sababu timu hiyo haikukamilisha taratibu.
“Polisi walifanikiwa kukata rufaa yao ndani ya muda, lakini bahati mbaya kitu kimoja tu, hawakulipa ada, hivyo rufaa yao haikusikilizwa kwa kuwa ilikuwa ipo kinyume cha utaratibu,”alisema Lucas.
Pamoja na hayo, Msemaji huyo wa TFF akasema kwamba hata kama rufaa hiyo ingesikilizwa Polisi Dar wasingeshinda kwa sababu kanuni za Kombe la ASFC hazikuwazuia Simba kumtumia mchezaji huyo.
Akifafanua, Lucas alisema kwamba adhabu zote za michuano hiyo hufanya kazi katika msimu husika pekee na kwamba kila msimu mpya mambo huanza upya.

No comments:

Post a Comment