KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 24, 2017

AZAM YAZIFUATA SIMBA NA YANGA HATUA YA MTOANO KOMBE LA SHIRIKISHO



AZAM FC imeungana na Simba na Yanga kusonga mbele katika michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho, baada ya kuichapa Cosmopolitan mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Kutokana na ushindi huo wa mechi hiyo ya raundi ya tano, Azam sasa itaungana na Simba na Yanga kwenye hatua ya 16 ya mtoano.

Yanga ilisonga mbele wiki iliyopita baada ya kuitandika Ashanti mabao 4-1 kwenye Uwanja wa Uhuru wakati Simba iliichapa Polisi Dar mabao 2-0 kwenye uwanja huo huo.

Nahodha John Bocco alifungua biashara kwa Azam dakika ya 69 baada ya kuifungia bao lake la kwanza kabla ya chipukizi Shabani Iddi kuongeza la pili dakika ya 76.

Cosmopolitan, moja ya timu kongwe za soka nchini, ilipata bao la kujifariji dakika ya 78 kupitia kwa Fidelis Kyanga kabla ya Azam kuongeza la tatu dakika ya 80 kupitia kwa Joseph Mahundi.

No comments:

Post a Comment