KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 3, 2017

TFF YAVUNJA MKATABA WA MKWASA KUINOA TAIFA STARS, YAKABIDHI MIKOBA KWA MAYANGA


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limetangaza kuvunja rasmi mkataba wa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars.

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas, amesema leo kuwa, mkataba huo ulivunjwa rasmi jana, baada ya kufanyika kwa kikao kati ya uongozi wa shirikisho hilo na kocha huyo.

Kwa mujibu wa Lucas, mkataba wa Mkwasa ulitarajiwa kumalizika Machi, mwaka huu.

Alipoulizwa kuhusu madai ya kocha huyo, Lucas alisema anachofahamu ni kwamba alishalipwa madai yake yote ya mishahara na kwamba, kilichobaki ni malipo ya miezi mitatu.

Akizungumzia uamuzi huo wa TFF, Boniface alithibitisha kufanyika kwa mazungumzo kati yake na shirikisho hilo kuhusu kukatisha mkataba wake.

Alisema katika mazungumzo hayo, TFF imekubali kumlipa mishahara yake iliyobaki ya miezi mitatu kwa awamu mbili tofauti.

Boniface alisema awamu ya kwanza atalipwa mwishoni mwa mwezi huu na awamu ya pili atalipwa mwezi ujao.

Kocha huyo alisema pia kuwa, alikubaliana na TFF kuhusu kupunguzwa kwa malipo ya mshahara wake wa kila mwezi kutokana na shirikisho hilo kutokuwa na uwezo kifedha.

"Katika mazungumzo yangu na TFF, waliniomba kupunguza kiwango cha malipo ya mshahara wangu wa kila mwezi kwa vile hawana uwezo kifedha. Nami kwa sababu ya kutambua ukweli huo na pia uzalendo wangu kwa taifa, nilikubaliana nao kuhusu uamuzi huo,"alisema.

Awali, Mkwasa alitakiwa kulipwa zaidi ya sh. milioni 30,kwa mwezi, kama alivyokuwa akilipwa kocha wa zamani. Hata hivyo, Mkwasa hakuwa tayari kuweka wazi kuhusu kiwango kilichopunguzwa.

Wakati huo huo, TFF  imemteua Salum Mayanga kuwa kocha wa muda  (Interim coach), wa Taifa Stars.

Mayanga anachukua nafasi ya Mkwasa, ambaye mkataba wake unafikia mwisho Machi, mwaka huu.

Kati ya majukumu yake yatakuwa ni kuandaa kikosi cha timu ya Taifa kwa ajili ya hatua ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2019, ambazo mechi za awali zitanza mapema mwaka huu.

Pia, Mayanga atakuwa na jukumu la kuandaa kikosi cha wachezaji wa ndani kwa ajili ya hatua ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi ya ndani (CHAN).

TFF inamshukuru Mkwasa kwa utumishi katika nafasi hiyo ulioanza Julai, 2015 na kumtakia mafanikio katika mipango yake inayofuata.

No comments:

Post a Comment