KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 17, 2017

YANGA YAIKARIBIA SIMBA, YAITUNGUA MAJIMAJI BAO 1-0


MABINGWA watetezi Yanga, leo wameichapa Majimaji bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Matokeo hayo yameiwezesha Yanga iwe nyuma ya vinara Simba kwa tofauti ya pointi moja. Simba inaongoza kwa kuwa na pointi 44, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 43.

Kiungo Deus Kaseke ndiye aliyeiwezesha Yanga kutoka uwanjani na pointi zote tatu, baada ya kuifungia bao hilo la pekee dakika ya 14, baada ya kipa Agathon Athony kupangua vibaya krosi iliyopigwa na Haruna Niyonzima.

Ligi Kuu itaendelea tena kesho kwa michezo miwili, Simba wakiwa wageni wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Azam FC wakiwa wenyeji wa Mbeya City, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment