KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 30, 2017

YANGA YAIENGUA SIMBA KILELENI MWA LIGI KUU


KIUNGO wa kimataifa wa Zambia, Obrey Chirwa jana aliipa furaha Yanga baada ya kuifungia mabao mawili, ilipoilaza Mwadui mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mechi hiyo ya ligi kuu ya Tanzania Bara, Chirwa aliyekuwa ameingia kipindi cha pili, alifunga mabao hayo dakika ya 69 na 82 na kuamsha shangwe kutoka kwa mashabiki wa Yanga.

Ushindi huo uliiwezesha Yanga kuiengua Simba kileleni mwa ligi kuu, ikiwa sasa inaongoza kwa pointi 46 baada ya kucheza mechi 20, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 45.

Chirwa, ambaye aliingia kuchukua nafasi ya Haruna Niyonzima, alifunga bao la kwanza kwa shuti kali baada ya kuuwani mpira uliopanguliwa vibaya na kipa Shaaban Kado wa Mwadui.

Mzambia huyo aliongeza furaha mashabiki wa Yanga kwa kufunga bao la pili kwa shuti lingine kali, kufuatia kupewa pasi ya kichwa na kiungo Thabani Kamusoko.

No comments:

Post a Comment