KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, January 29, 2017

AZAM YAITAMBIA TENA SIMBA




BAO lililofungwa na mshambuliaji John Bocco, jana liliiwezesha Azam kuichapa Simba bao 1-0 katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara, iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo ulikuwa wa pili mfululizo kwa Azam dhidi ya Simba katika siku za hivi karibuni. Azam pia iliichapa Simba bao 1-0 katika mechi ya fainali ya Kombe la Mapinduzi, iliyochezwa mapema mwezi huu kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.

Bocco, ambaye pia ni nahodha wa Azam, alifunga bao hilo la pekee dakika ya 70 baada ya kumtoka beki Method Mwanjali wa Simba ndani ya eneo la hatari.

Kipigo hicho kimepunguza matumaini ya Simba kutwaa ubingwa wa ligi hiyo kwani huenda ikapokonywa uongozi na Yanga, iwapo mabingwa hao watetezi wataifunga Mwadui leo.

No comments:

Post a Comment