KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 25, 2017

MECHI ZINGINE ZA KOMBE LA SHIRIKISHO KUPIGWA TENA LEO


Mechi za raundi ya tano ya mechi za Kombe la Shirikisho la Azam 2016/17 (Azam Sports Federation Cup – ASFC), zitaendelea kesho Jamatano Januari 25, 2017 kwa timu za Singida United na Kagera Sugar kucheza kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

Mchezo mwingine utakaozikutanisha timu za The Mighty Elephant ya Songea na Mashujaa ya Kigoma katika mchezo utakaofanyika Uwanja Majimaji mjini Songea.

Katika mchezo huo ambao uliahirishwa Jumatano iliyopita, mshindi wa kesho ndiye atacheza na Majimaji katika tarehe mpya itakayotangazwa hapo baadaye kama ilivyo kwa mechi kati ya African Lyon na Mshikamano.



No comments:

Post a Comment