KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2017

YANGA YAZIDI KUTAKATA KOMBE LA MAPINDUZI


YANGA jana iliendelea kung'ara katika michuano ya soka ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa Zimanimoto ya Zanzibar mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa jioni kwenye Uwanja wa Amaan, Unguja.

Ushindi huo ulikuwa wa pili mfululizo kwa Yanga na uliiwezesha kuongoza kundi B ikiwa na pointi sita baada ya kucheza mechi mbili, ikifuatiwa na Azam. Timu hizo mbili zinatofautiana kwa mabao ya kufunga.

Mshambuliaji Simon Msuva aliibuka shujaa wa Yanga baada ya kuifungia mabao yote mawili na kuiwezesha timu hiyo kukata tiketi ya kucheza robo fainali.

Alifunga bao la kwanza dakika ya 11 baada ya kumvisha kanzu kipa Mwinyi Hamisi wa Zimamoto. Awali, alipokea pasi kutoka kwa Haruna Niyonzima.

Msuva aliiongezea Yanga bao la pili dakika ya 21 baada ya kuwatoka mabeki wa Zimamoto na kumpiga chenga kipa Hamisi wa Zimamoto.


No comments:

Post a Comment