KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 1, 2013

SIMBA, YANGA ZAINGIZA MIL 182/-



Mechi za Yanga na Simba za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zilizochezwa wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam zimeingiza jumla ya sh. 182,103,000.

Yanga katika mechi yake dhidi ya Ruvu Shooting iliyochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa bao 1-0 imeingiza sh. 94,202,000.

Watazamaji 16,492 walikata tiketi kushuhudia pambano hilo ambapo kila klabu ilipata mgawo wa sh. 22,630,921.58. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000, na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 14,369,796.61.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 11,507,248.26, tiketi sh. 3,117,215, gharama za mechi sh. 6,904,348.96, Kamati ya Ligi sh. 6,904,348.96, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,452,174.48 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,685,024.59.

Nayo Simba ambayo iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu katika mechi iliyochezwa Jumapili (Septemba 29 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 87,901,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 41 walikuwa 15,780. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 21,051,025.92 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 13,408,627.12.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 10,703,911.48, tiketi sh. 3,132,963, gharama za mechi sh. 6,422,346.89, Kamati ya Ligi sh. 6,422,346.89, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 3,211,173.44, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,248,789.67 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 1,248,789.67.

Wakati huo huo, mechi ya ligi hiyo kati ya Mbeya City na Coastal Union  iliyochezwa Jumamosi (Septemba 28 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya imeingiza sh. 16,959,000 huku kila klabu ikipata sh. 4,035,229.

Mgawo wa mechi hiyo ulikuwa ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 2,586,966, uwanja sh. 2,051,811.57, tiketi sh. 696,290, gharama za mechi sh. 1,231,086, Kamati ya Ligi sh. 1,231,086, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 615,543, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA) sh. 478,756.

No comments:

Post a Comment