KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 7, 2010

VUMBI AFYATUA NNE MPYA



Na Badru Kimwaga
MWANAMUZIKI mahiri, aliyewahi kuipigia bendi ya Marquiz Original, Alain Dekula 'Vumbi', amefyatua nyimbo mpya nne ikiwa ni maandalizi ya kupakua albamu yake ya tatu mpya.

Akizungumza na mtandao huu juzi jijini akiwa kwenye mapumziko, Vumbi alisema nyimbo hizo nne zimerekodiwa nchini Sweden anapofanyia shughuli zake za muziki na kwamba ni mbio zake za kutoa albamu yake ya tatu nje ya bendi yake ya Makonde.

Vumbi alisema nyingine nne zitakazokamilisha jumla ya nyimbo nane za albamu hiyo mpya, tayari zimeshatungwa mashairi yake, lakini hazijapewa jina hadi atakapoingia studio kuzirekodi.

"Baada ya kutamba na albamu za Sultan Qaboos na Rumaliza ambayo bado ipo kwenye chati na
nimeleta video yake ili Watanzania nao mpate uhondo, nimeanza maandalizi ya albamu ya tatu,
ambayo itakuwa na jumla ya nyimbo nane," alisema Vumbi.

Mkali huyo wa kucharaza gita la solo, alizitaja nyimbo zilizokamilika ni Mawele, Tenda Wema, Coco na Dar Night maarufu kama No Stop.

Vumbi aliyeondoka nchini mwaka 1991 baada ya kukaa na Marquiz kwa karibu miaka nane, alisema nyimbo hizo za awali anatarajia kuanza kuzisambaza kenye blog yake pamoja na kwenye vituo vya redio vya nchi mbalimbali kwa lengo la kuzitangaza.

Aliongeza kuwa kama albamu zake za awali, hata hiyo ya tatu atafyatua kwa kushirikiana na baadhi ya wanamuziki wa bendi yake ya Makonde, akiwemo Mganda Sammy Kasule, Bobo Sukari aliyewahi kutamba Marquiz kabla ya kuondoka nae kwenda Sweden.

Hata hivyo Vumbi alisema Bobo Sukari kwa sasa amejiondoa kwenye bendi yao yenye wasanii nane wakiwemo wanne wazungu kutokana na kile alichokataa kukieleza."

Kwa sasa Bobo hayupo nasi, ila siwezi kusema ni kwa ajili ya nini, lakini tunaendelea kuwasiliana na atashiriki pia katika albamu hii ya tatu," alisema Vumbi.

No comments:

Post a Comment