KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 14, 2010

Rooney atoa changamoto kwa Ferguson



LONDON, England

MSHAMBULIAJI Wayne Rooney wa Manchester United amesema anaamini, klabu hiyo inahitaji wachezaji wawili zaidi wa kiwango cha juu katika ligi ya msimu ujao.

Rooney alisema mjini hapa juzi kuwa, mmoja wa wachezaji hao anapaswa kuwa mshambuliaji, ili kukiongezea nguvu kikosi hicho baada ya kupokonywa taji la ligi kuu ya England msimu huu na Chelsea.

Mshambuliaji huyo ameonyesha kiwango cha juu msimu huu, ambapo ameifungia Manchester United mabao 34.

Hata hivyo, Rooney alipatwa na mkosi mwishoni mwa ligi hiyo baada ya kuumia kifundo cha mguu na kukaa benchi kwenye mechi kadhaa.

Rooney ndiye aliyekuwa tegemeo kubwa la Manchester United katika ufungaji magoli msimu huu, kufuatia kuondoka kwa Cristiano Ronaldo na Carlos Tevez msimu uliopita.

Licha ya Manchester United kushika nafasi ya pili msimu huu, nyuma ya Chelsea kwa tofauti ya pointi moja, Rooney alisema bado kuna umuhimu wa Kocha Sir Alex Ferguson kuongeza nyota wawili msimu ujao.

“Kama tutaweza kuongeza wachezaji wawili wenye majina makubwa, itatupa nafasi kubwa ya kurejesha taji la ligi kuu,”alisema Rooney.

“Kama utatazama timu ya mwaka 1999 iliyoshinda mataji matatu, tulikuwa na washambuliaji wanne na wote walikuwa na uwezo wa kufunga mabao,”aliongeza.

“Kwa sasa nipo mimi, Berbatov na Owen. Yupo pia Macheda, lakini kama tunaweza kumpata mwingine zaidi, itatuongezea nguvu zaidi,”alisema.

Mbali na Rooney, wachezaji wengine wanaounda safu ya ushambuliaji ya Manchester United kwa sasa ni Dimitar Berbatov, Michael Owen na chipukizi Federico Macheda na Mame Biram Diouf.

No comments:

Post a Comment