KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 7, 2010

MERCY KUSUJUDU VIDEON

Na Badru Kimwaga
MSANII anayekuja juu katika muziki wa Injili nchini, Mercy Margareth Mbilu ameanza kurekodi video ya nyimbo za albamu yake ya kwanza iitwayo Ukinisujudia.
Kazi ya 'kushuti' video hiyo ilianza mapema wiki hii, ingawa imesimama kupisha hali ya mvua inayoendelea jijini Dar es Salaam na Mercy alisema itaendelea tena mvua zikitulia na huenda kabla ya kumalizika kwa mwezi huu wa Mei, video hiyo ikawa mitaani.
Mercy aliuambia mtandao huu kuwa, ameamua kufyatua video ya albamu hiyo ili kuweza kuiingiza sokoni sambamba na albamu kamili kutoa fursa kwa wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili kuzipata zote kwa pamoja.
"Nimeanza kushuti, vieo ya albamu yangu ya Ukinisujudia kwa lengo la kutaka kuziingiza sokoni pamoja na audio, ili kila mpenzi apate kile roho inapenda na mipango huenda ikakamilika katikati ya mwezi Mei," alisema Mercy.
Alizitaja nyimbo zilizoanza kurekodiwa video kuwa ni Ukinisujudia, Utafuteni Upendo na Nitakusifu Mungu wa Rehema.
"Hizo ndizo nilizoanza nazo na mvua zikiacha kunyesha na hali ya hewa kuwa nzuri nitamalizia nyimbo tano zilizosalia ambazo ni Zakayo, Na Hili Bwana Nishindie, Nitakukimbilia, Bwana Yesu Atasimama na Unirehemu Ewe Yesu.
Mercy alisema amepanga video yake irekodiwa katika ubora na kiwango cha hali ya juu ili kuweza kuteka soko la muziki huo ambalo kwa sasa lina ushindani mkubwa.
Kampuni inayomfanyia kazi hiyo ya kurekodi video hiyo ni moja ya kampuni maarufu za kazi hiyo zilizopo jijini Dar es Salaam ambayo imewarekodia wasanii mbalimbali nyota wa muziki huo wa Injili na ule wa kizazi kipya.

No comments:

Post a Comment