KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 18, 2013

MECHI MBILI ZA YANGA KUIVUA UBINGWA SIMBA


UBINGWA wa michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara umezidi kunukia kwa Yanga baada ya kuichapa Ruvu Shooting bao 1-0 katika mechi iliyopigwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo umeiwezesha Yanga kuwa na pointi 48 baada ya kucheza mechi 20 na sasa inahitaji kushinda mechi mbili ili iweze kuwavua ubingwa, mabingwa watetezi Simba.

Iwapo Yanga itashinda mechi hizo mbili, itafikisha pointi 54, ambazo Simba haitaweza kuzifikia hata kama itashinda mechi zake sita zilizosalia. Simba itakuwa na uwezo wa kufikisha pointi 52.

Katika mechi zake mbili zijazo, Yanga itakipiga na Polisi Morogoro Machi 30 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro kabla ya kukipiga na JKT Oljoro Aprili 10 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Ruvu Shooting na Yanga iliyochezwa jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 62,228,000 kutokana na watazamaji 10,929.

Viingilio katika mechi hiyo namba 146 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 14,336,764.95 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,492,406.78.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,289,880.48, tiketi sh. 4,136,390, gharama za mechi sh. 4,373,928.29, Kamati ya Ligi sh. 4,373,928.29, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,186,964.14, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 850,486.06 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 850,486.06.



No comments:

Post a Comment