KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 18, 2013

AZAM YAJIWEKA PAZURI KOMBE LA SHIRIKISHO




AZAM FC imejiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza raundi ya tatu ya michuano ya soka ya Kombe la Shirikisho baada ya kuichapa Barrack Young Controllers ya Liberia mabao 2-1.

Katika mechi hiyo ya awali ya raundi ya pili iliyochezwa jana kwenye uwanja wa Antonette Tubman mjini Monrovia, Azam ilikwenda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao 1-0.

Kwa matokeo hayo, Azam sasa inahitaji sare yoyote katika mechi ya marudiano itakayochezwa wiki mbili zijazo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mshambuliaji Seif Abdalla Karihe aliibuka shujaa wa Azam baada ya kuifungia bao la pili na la ushindi dakika ya 90. Seif aliingia uwanjani dakika 10 kabla ya kufunga bao hilo, akichukua nafasi ya Kipre Tchetche.

Barrack ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 44 lililofungwa na Junior Barshall.

Bao la kusawazisha la Azam lilifungwa na Humphrey Mieno dakika 10 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Jabir Azizi na Khamis Mcha.

No comments:

Post a Comment